Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Fahamu madhara ya kula chipsi

E3d80ea8cd7257a4bf73826bd7509483 1 Fahamu madhara ya kula chipsi

Tue, 30 Aug 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kiukweli katika vyakula vitamu duniani na vinavyopendwa haswaa na watu duniani usiposema chipsi utakuwa mtu waajabu sana. Chipsi haziliki bongo tu ata ughaibuni chips zinalika sana na zinapendwa haswaa, chipsi zinaenda na vitu vingi kama chipsi yai, chipsi kuku na kadharika.

Hizi ndio athari za ulaji wa chipsi.

Husababisha magonjwa ya moyo Kwa kuzingatia ukweli kwamba zimekaangwa sana katika mafuta ya hidrojeni, chipsi huja na kiasi kikubwa cha mafuta, ambayo huongeza cholesterol yako mbaya na kupunguza cholesterol yako nzuri. Athari kubwa ya hii ni kwamba utaongeza hatari ya ugonjwa wa moyo.

Ulaji wa chipsi husababisha magonjwa ya moyo

Hupunguza kinga ya mwili Kulingana na utafiti uliochapishwa katika jarida la Current Opinion in Clinical Nutrition & Metabolic Care, kula chakula chenye mafuta mengi na vyakula vyakukaanga vingi unaweza kuwa unaharibu utumbo wako kwa kuongeza bakteria wasio na afya na kupunguza bakteria wa afya ya mwili wako.

Kwa kuzingatia jukumu la utumbo katika kusaidia kufahamisha mfumo wa kinga ya mwili wako, unaweza kuwa unaweka mwili wako hatarini kupata magonjwa.

Huongeza uzito wa mwili Vyakula vya kukaangwa katika mafuta, huwa mabomu ya kalori, na kusababisha kupata uzito.

Utafiti uliochapishwa katika jarida la The American Journal of Clinical Nutrition uligundua kuwa kula vyakula vya kukaanga kunahusishwa moja kwa moja na unene kupita kiasi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live