Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Daktari aelezea dhana majani ya chai kusababisha presha

HBP.png Daktari aelezea dhana majani ya chai kusababisha presha

Fri, 5 Jun 2020 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

SHINIKIZO la juu la damu (presha ya kupanda) hutokea wakati nguvu ya msukumo wa damu katika mishipa ya moyo huwa kubwa kuliko kawaida.

Ongezeko hilo husababisha moyo kufanya kazi kupita kiasi ili kusukuma damu katika mishipa ya damu.

Kwa kawaida ugonjwa wa presha hauna dalili ili ukidumu kwa muda mrefu bila ya tiba kuna madhara makubwa kiafya.

Wataalamu wa afya wanabainisha aina mbili za presha ambazo ni ya kurithi na inayosababishwa na magonjwa mbalimbali.

Kwa mujibu wa wataalamu wa afya, asilimia 95 ya wagonjwa wa presha ya kupanda hawana sababu zinazojulikana kisayansi.

Mara nyingi sababu zinazoainishwa ni historia ya ugonjwa katika familia, uzito mkubwa matumizi ya chumvi nyingi, kutokufanya mazoezi, uvutaji sigara, ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na umri mkubwa.

Asilimia kubwa ya watu wanaopata ugonjwa presha ya kupanda huwa wanakuwa katika husumbuliwa na magonjwa mbalimbali kama figo, mishipa ya moyo na mfumo wa homoni.

Katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) tangu ilipoanzishwa Septemba 2015 hadi Aprili 2020 kati ya wagonjwa 334,774 waliotibiwa, asilimia 66 ya wagonjwa walikuwa na tatizo la presha ya kupanda.

Idadi hiyo ya wagonjwa inadhihirisha kuwa bado kunauhitaji mkubwa wa elimu kwa jamii kuhusu jinsi ya kuweza kuepuka hatari zinazoweza kusababisha shikizo la damu la juu.

Katika kuadhimisha siku ya presha ya kupanda kila ifikapo Mei 17, Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete iliamua kutoa elimu kwa jamii kuhusu ugonjwa huo na jinsi ya kuuepuka.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa taasisis hiyo, Dk. Samweli Rweyemamu, anasema wamedhamiria ni kutaka jamii kujua sababu hatarishi zinazoweza kusababisha mtu kupata presha ya kupanda.

“Tunaendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusu ‘risk factor’ zinazosababisha shinikizo la juu la damu pia tumeweza kueleza kuwa kuna aina mbili ambazo ni sababu za kurithi na mazingira.

“Sababu zinazotokana na mazingira zinaweza kuzuilika lakini sababu za kurithi kuzuilika inakuwa vigumu au hata ile ya umri kunzia miaka zaidi 65 nafasi ya kupata presha inakuwa kubwa,” anaeleza Dk. Rweyemamu.

MATUMIZI DAWA NGUVU ZA KIUME HATARI

Kwa mujibu wa Dk. Rweyemamu, moja ya matokeo hasi ya matumizi ya dawa za presha na zile za moyo huweza kusababisha kupungua kwa hamu ya ngono (sexual respond).

Anasema hali hiyo imekuwa ikiwakumba wanaume wengi wanaotumia dawa hizo na amekuwa akipata malalamiko ya mara kwa mara.

“Mtu mwenye presha anao uwezekano mkubwa wa kupata matatizo ya moyo na kulingana na tunavyoendelea kupata wagonjwa inaonekana watu wenye shida ya presha na magonjwa ya moyo kwa ujumla ‘side effect’ ya dawa au hata ugonjwa ni kuwa na uwezo mdogo wa kufanya ngono na inaonekana shida hii ni kubwa kwa sababu wagonjwa tunaowaona wengi hasa wanaume huwa wanalalamikia suala hilo.

“Kutokana na suala hilo kuwa tatizo, watu wanatakiwa kujua jinsi ya kuishi nalo kwa sababu shida imeshajitokeza, ukisema usimeze dawa maana yake utapata madhara makubwa kama kupata kiharusi (stroke), moyo na figo kushindwa kufanya kazi, kwahiyo utakuta madhara ni makubwa zaidi,” anasema Dk. Rweyemamu.

Anawasisitiza watu wanaotumia dawa hizo, kuepuka kutumia dawa za kuongeza nguvu za kiume kwa sababu madhara yanaweza kuwa makubwa zaidi kwa afya ya mtumiaji.

“Kikubwa tunawasihi watu wasinunue dawa hovyo mitaani, hasa zinazoongeza nguvu za kiume kwa sababu ukizichangaya na dawa za moyo bila ushauri wa daktari kwa sababu zinasababisha madhara makubwa, inaweza kushusha presha ghafla mtu akapoteza maisha, hili ni jambo ambalo watu wanatakiwa wafahamu kwa sababu inaweza kuzidi hata presha yenyewe,” anasema Dk. Rweyemamu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live