Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Daktari: Jiulize kwanini unahisi una corona

99019 Pic+corona Daktari: Jiulize kwanini unahisi una corona

Mon, 16 Mar 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Marekani. Wakati maambukizi ya virusi vya corona vilivyoanzia China vikiendelea kusambaa katika nchi mbalimbali duniani, wataalamu wa afya wanasema kuna baadhi ya watu hawajui hatua za kuchukua endapo wanakuwa na dalili za ugonjwa huo.

Inaelezwa kuwa kumekuwa na mkanganyiko kidogo kwa baadhi ya watu kuhusu hatua gani za kufuata na wapi pa kupimwa na kutibiwa.

Mkurugenzi wa matibabu wa Shirika la Taifa la Magonjwa ya kuambukiza ambaye pia ni profesa katika Kituo cha Matibabu cha Chuo Kikuu cha Vanderbilt, Dk William Schaffner, anasema, “kitu cha kwanza unachotakiwa kufanya ni kujiuliza kwanini unadhani una virusi vya corona?

“Vipi kuhusu mabadiliko ya hali yako, umerudi kutoka nchi fulani na ulisalimiana na mtu kutoka nchi nyingine ambako kuna maambukizi ya virusi vya corona?

Wataalamu hao wanasema kitu cha kukitilia shaka zaidi ni kwamba kama unasumbuliwa na magonjwa ya moyo, kisukari na mapafu, utakuwa katika hatari zaidi ya ugonjwa huo.

Wanasema hata kama hauumwi corona, ila una dalili zote za ugonjwa huo, unapaswa kuwasiliana na daktari kwa ushauri zaidi.

Pia Soma

Advertisement
Dk Sheldon Campbell ambaye ni mtaalamu wa dawa anasema: “Kama unahisi hauumwi corona, muite daktari atathimini afya yako.”

Chanzo: mwananchi.co.tz