Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk Dorothy Gwajima amewaagiza maafisa jamii nchini kote kuhakikisha wanawezesha upatikanaji wa haki kwa wakati kwa wanaofanyiwa vitendo vya ukatili.
Gwajima amebainisha hayo leo Jijini Dodoma alipozungumza na vyombo vya habari kuhusiana na mwenendo wa vitendo vya ukatili hapa nchini.
“Niwaase maafisa jamii katika halmashauri zote nchini kushughulikia ipasavyo ukatili dhidi ya wanawake, wanaume, watoto na wazee kwa kuhakikisha haki za wananchi wanaofanyiwa vitendo hivyo ikiwemo makundi tete zinapatikana kwa wakati” amesema Dk Gwajima.