Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

CT-Scan Muhimbili yaharibika, wagonjwa wapelekwa Moi na Mloganzila

101848 Pic+muhimbili CT-Scan Muhimbili yaharibika, wagonjwa wapelekwa Moi na Mloganzila

Fri, 10 Apr 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imesema mashine yake ya  CT Scan haifanyi kazi na wagonjwa wa dharura  wanaohitaji huduma hiyo wanapelekwa Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu Muhimbili (Moi) na hospitali ya Mloganzila.

Akizungumza na Mwananchi leo Jumatano Aprili 8, 2020  mkuu wa kitengo cha mawasiliano katika hospitali hiyo,  Aminiel Aligaesha amesema mashine hiyo haifanyi kazi tangu  Aprili 7, 2020, kubainisha kuwa huduma zimesimama katika hospitali hiyo.

“Chanzo ni kuharibika kwa kifaa kinachotoa mionzi ya kupiga picha (CT- scan x-ray tube). Kumekuwa na usumbufu lakini kifaa kilichoharibika tayari kimeagizwa nchini Ujerumani.”

Chanzo: mwananchi.co.tz