Thu, 2 Jun 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Serikali imeandaa kanuni za kudhibiti bei za dawa na tayari zimewasilishwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Naibu Waziri wa Afya, Godwin Mollel, ameyasema hayo bungeni mjini Dodoma leo akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum, Mwanaisha Ulenge aliyetaka kujua kuhusu bei elekezi ya vifaa tiba haswa vya macho, pua na koo.
Mollel amesema bei elekezi za vifaa tiba zitaandaliwa mara baada ya kukamilika kwa kanuni za bei za dawa elekezi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live