Waziri wa Afya, maendeleo ya jamii, jinsia wazee na watoto, Dk Dorothy Gwajima amewataka watendaji wa huduma za afya kufanya kazi kwa bidhii kwa lengo la kuisaidia jamii kuepuka kusafiri kwenda nje ya nchi kutafuta huduma za afya.
Akizungumza jijini Mwanza katika Kongamano na Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Wataalamu wa Mionzi na Tiba, Dk Gwajima amesema Serikali imeboresha huduma za afya kwa kusambaza vifaa tiba, hivyo ni jukumu la watendaji kuhakikisha wanatoa huduma bora.
Aidha, amewakata kufanya kazi kwa ushindani katika utoaji wa huduma kwa jamii ili kukabiliana soko kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambao wanatumia wataalamu wenye viwango vya kimataifa ili kuwezesha wananchi wanapata huduma inayostahili