Mon, 16 Mar 2020
Chanzo: mwananchi.co.tz
Uingereza. Je, unajua kwamba unapokunywa kahawa kila siku unakuza afya yako na kukusaidia uishi maisha marefu?
Utafiti uliofanyika nchini Uingereza na kuhusisha takribani watu 20,000 umeeleza kuwa angalau watu wanaokunywa vikombe vinne vya kahawa kila siku wanapunguza uwezekano wa kufa mapema kuliko wale ambao hawanywi kahawa.
Msemaji wa Taasisi ya Taifa ya Kahawa, Joe DeRupo alisema kahawa pia imeonekana kupunguza hatari ya kupata magonjwa mbalimbali ikiwamo kisukari aina ya pili, saratani ya ngozi.
Chanzo: mwananchi.co.tz