Kijamii

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Lifestyle

SIL

MenuKijamiiMaoni
Articles

Uchambuzi wa Simba Vs Young Africans

FB IMG 1625331467002 Uchambuzi wa Simba Vs Young Africans

Sun, 4 Jul 2021 Chanzo: dar24.com

DAKIKA 90 – KARIAKOO DERBY

Dakika 45 za kipindi cha kwanza bora kwa Yanga SC, Yani ile mpira umeanza Yanga walikuwa kweli kweli wameianza mechi, walicheza kiume, hawakutaka kuwa slow, walienda kwa nguvu

Simba hawakuweza kutuliza presha ya Yanga mpaka wanafungwa goli, hilo ndilo lilikuwa kosa kubwa la Simba na ubora maridadi wa Yanga

Feisal Salum alicheza kwa kuheshimu nafasi yake, alivizia pocket space sana, kila Yanga walipopora mpira aliuomba kwa haraka na kugeuka

Kwa jinsi Yacouba alivyokuwa akikimbia, amewapa sana mabeki wa Simba, dakika mbili kulia mara kushoto mara kati, hii ni nightmare kwa Beki yeyote

Kiufupi Yanga kipindi cha kwanza walikuwa na wakati mzuri, walipiga progressive passes ila Simba walipiga possessive passes, faida hapo ni kwa wananchi

Kipindi cha pili kumbe Simba walichokuwa wanakitafuta walikuwa wamekikalia, akaingia Bwallya, huyu ndie aliipa Simba walichofikiria sio walichocheza

Mechi ikaamia kwa Simba, kwa upande wao walifanya kila kitu ila hawakufunga goli

Kama ilivyo kawaida ya mapacha hivi karibuni, kipindi cha kwanza alikichukua Yanga na cha pili alichukua Simba, ila Yanga wao hawakukichezea walikitumia, Simba alikichukua na kukipapasa

Kwa mara nyingine tena tunakuja kuona wananchi wanawazidi Simba kwenye swala la kujitoa, achilia mbali mbinu, hizo tupa kule

Ila pale Simba alipotaka goli Yanga alimpiga pini na kuzuia kwa nguvu, ila pale Yanga alipotaka goli Simba alishindwa kuhimili na Yanga alilipata

NB: Hata mkichukua ubingwa ila ubingwa ni butu

Columnist: dar24.com