Kijamii

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Lifestyle

SIL

MenuKijamiiMaoni
Articles

UCHAMBUZI: Simba walijifunza, wametekeleza msimu huu

Simba Noti Pic Data UCHAMBUZI: Simba walijifunza, wametekeleza msimu huu

Mon, 1 Mar 2021 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

Hakuna kitu muhimu kwa binadamu kama kujifunza na kujua, kwani siku zote kujifunza sio lazima kujua ndio maana kuna wengine wanajifunza lakini hawafanikiwi kujua, hivyo si kila anayejifunza hujua kile alichojifunza.

Nasema hivyo kwa sababu katika mchezo wa soka pia somo hilo na ni miongoni mwa masomo muhimu katika mafunzo yote kuanzia ya wachezaji, makocha hadi waamuzi ambapo hufundishwa kuwa katika tasnia hii kila siku ya mechi au mazoezi huwa ni siku ya kujifunza kitu kipya hivyo tunatakiwa kujifunza na kukijua ili kikitokea siku nyingine tuweze kukabiliana nacho.

Ni kutokana na tofauti hiyo iliyopo kati ya kujifunza kitu na kujua ndio maana huwa linakuja suala la uzoefu kwa wachezaji ambalo hutofautisha thamani ya mchezaji kati ya mzoefu na yule asiyekuwa na uzoefu ambapo mwenye uzoefu huwa na manufaa kwa timu kupitia ujuzi alioupata katika muda aliokuwa akicheza na kukutana na changamoto mbalimbali ambazo ndizo zilizomuongezea ujuzi baada ya kujifunza.

Nazungumza hivyo baada ya kuona wiki iliyopita timu ya Simba ikipata ushindi katika mechi ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika dhidi ya mabingwa watetezi Al Ahly kutoka nchini Misri, huku washabiki na wafuatiliaji wote wa mechi wakiridhishwa na kiwango kilichoonyeshwa na Simba katika mchezo huo.

Moja kati ya sababu kubwa iliyowafanya Simba kuweza kupata matokeo hayo ni uzoefu walioupata kupitia mashindano hayohayo msimu uliopita na kuweza kujua kile kinachotakiwa kufanyika ili kufika mbali katika mashindano.

Ni kweli na hapana shaka kuwa miongoni mwa mechi kubwa na zilizoweka historia kwa Simba ni mechi dhidi ya Al Ahly ambayo ilikuwa ikifuatiliwa na wadau wengi wa soka kutoka kila kona ya dunia.

Columnist: mwanaspoti.co.tz