Kijamii

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Lifestyle

SIL

MenuKijamiiMaoni
Articles

Tafsiri ya hati yenye mashaka Dar

Cag Kichere Gh CAG Kichere akikabidhi ripoti yake kwa Rais Samia

Fri, 1 Apr 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

RIPOTI ya CAG imetoa hati yenye mashaka katika ukaguzi wake wa hesabu za serikali kwa Jiji la Dar es Salaam.

Dar ni miongoni mwa taasisi na mashirika ya umma 999 yaliyokaguliwa na CAG kwa ripoti ya 2020-2021 na kuwepo kwenye orodha ya hati 19 zenye mashaka zilizotolewa.

Wengi wanaposikia hati yenye mashaka, wamekuwa hawaelewi mkaguzi anamaanisha nini katika ripoti.

Ufafanuzi wa tafsiri ya hati zinazotolewa na CAG ni huu:

Hati yenye mashaka inatolewa iwapo taarifa za fedha

hazikuonyesha usahihi, kutokukubaliana na uongozi au kukwazwa kwa mawanda ambapo athari yake ni kubwa lakini si muhimu na kwamba ukiacha athari zilizosababisha kutoa hati yenye shaka, taarifa za hesabu zimetengenezwa na kuwepo kutoelewana kwa maelezo ya viongozi husika.

Hati isiyoridhisha inatolewa pale ninapothibitisha kwamba, taarifa za fedha hazikutengenezwa kwa kufuata misingi ya inayokubalika ya utayarishaji wa

taarifa.

Hesabu zilizowasilishwa hazina maelezo ya kutosha ambayo

yanawezesha taarifa za fedha kuelezeka vizuri na kwa upana zaidi.

Hati mbaya au chafu hutolewa wakati uthibitisho wa ukaguzi ni wa

kutosha na hivyo kushindwa kutoa maoni juu ya taarifa za fedha

zilizowasilishwa.

Endapo taarifa za fedha zitakuwa na mapungufu makubwa basi hati chafu hutolewa.

Hati safi hutolewa baada ya ukaguzi kupitia nyaraka na kujilidhisha kuwa kla kitu kiko sawa.

Columnist: www.tanzaniaweb.live