Kijamii

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Lifestyle

SIL

MenuKijamiiMaoni
Articles

Skendo ya Walimu Kufanya Mapenzi na Wanafunzi Yatikisa

Wanafunzi.jpeg Skendo ya Walimu Kufanya Mapenzi na Wanafunzi Yatikisa

Fri, 31 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

MWAKA 2021 unapokaribia kutamatika, baadhi ya walimu wa shule mbalimbali wanauaga kwa skendo ya kujihusisha kimapenzi na wanafunzi wao.

Kuna baadhi ya walimu walinaswa laivu wakiwafanyia uchafu na wanafunzi wao, baadhi waliwaoa kabisa na wengine kulalamikiwa kuwaharibu wanafunzi wa kike kimyakimya.

Ripoti ya Serikali ya mwaka 2021, imesema, walimu 285 kati 10,115 walifikishwa katika Tume ya Utumishi wa Ualimu (TSC) kwa tuhuma za kujihusisha na mapenzi na wanafunzi katika kipindi cha miaka minne.

Ripoti hiyo ilitolewa Septemba 7, 2021 na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Ummy Mwalimu.

Skendo hii ya walimu kujihusisha kingono na wanafunzi wao ilithibitishwa pia na Mwenyekiti (TSC), Dk Willy Komba, jijini Dodoma alipozungumza na waandishi wa habari.

Hali inavyoonekana tatizo la mapenzi kati ya walimu na wanafunzi linakua, wewe kama mwananchi unadhani nini kinasababisha na kipi kifanyike 2022, ili walimu viwembe washike adabu yao?

Columnist: www.tanzaniaweb.live