Kijamii

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Lifestyle

SIL

MenuKijamiiMaoni
Articles

Simba bado mna meci 4 za kujitutumua

Simba Sc Caf.jpeg Kikosi cha Simba SC kilichoanza dhidi ya Raja Casablanca

Sun, 19 Feb 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Licha ya kupoteza mchezo wao wa jana kwenye dimba la Mkapa kwa mabao 0-3 dhidi ya Raja Casablanca ya Morocco, Simba SC wamebakiwa na michezo minne ya kujitutumua ili kufuzu hatua ya robo fainali.

Mchezo unaofuata ni dhidi ya Vipers ya Uganda ambao wana pointi 1, waliyoipata kwenye sare dhidi ya Horoya ya Guinea, hivyo Simba SC atahitaji amfunge Vipers nyumbani kwake na mchezo wa marudiano amfunge kwenye dimba la Mkapa ili afikishe pointi 6 zitakazo muweka nafasi nzuri zaidi.

Ikumbukwe pia Simba mchezo wake wa mwisho atamalizia nyumbani dhidi ya Horoya hivyo ili kuwa na matumaini zaidi ya kufuzu hatua ya robo fainali, anapaswa pia amfunge kwa mabo mengi zaidi Horoya ili endapo wataringana pointi na magoli ya kufunga na kufungwa, ile kanuni ya ‘head to head’ itahukumu nani anafuzu hatua inayofuata.

Ukiachana na matokeo ya mpira kutokufikirika, lakini bado Simba ana nafasi ya kusonga mbele kama akichanga karata zake vizuri. Kwani kilimfanya apoteze jana dhidi ya Raja ni Ubora wa wachezaji mmoja mmoja (Quality).

Ukizingatia Raja wanatoka nchi yenye kiwango kikubwa cha Soka iliyofika hatua ya robo fainali kombe la dunia 2022 nchini Qatar, hivyo wachezaji wao wengi wana ubora mkubwa sana ukilinganisha na wachezaji wa Simba.

Kundi la Simba linanifanya nirudi nyuma miaka 3 kwenye Ligi ya Mabingwa (CAFCL) ilikuwa kama hivi Simba alikuwa anaenda ugenini anachezea goli za kutosha lakini bado alijitutumua na kupata matokeo nyumbani.

Hata hivyo Mechi ya Mwisho ya kuamua nani anafuzu hatua ya robo fainali kati ya Simba vs AS Vita ambapo Francy Kazadi akiitanguliza Vita Club kwa bao la mapema tu, lakini Mohammed Hussein alisawazisha kabla ya Chama kufunga bao la pili dakika za jioni kabisa na kuwafanya Simba kufuzu hatua robo fainali.

Simba bado ana nafasi ya kusonga mbele ila awe makini tu asidondoshe pointi kwenye michezo yake mitatu dhidi ya Vipers nje ndani, na wa Horoya nyumba kwa Mkapa.

Columnist: www.tanzaniaweb.live