Ligi inayoenda kuanza msimu huu ni tofauti na ligi zilizotangulia, kuanzia kwenye uwezeshwaji, timu zimewezeshwa vilivyo na wadhamini wa Ligi.
Kwa hiyo wana kila sababu ya kufanya maandalizi, siku za nyuma kilichokuwa kinasababisha wakati mwingine ni rasilimali, unakuta timu haina rasimali fedha ya kufanya waweze kwenda kufanya Pre-season nje.
Mkitoka kwenda kufanya Pre-season ni gharama asilimia mia, kwaiyo kwasasa timu zina kianzio, kwaiyo walichokifanya ni sahihi
Kingine, siku hizi vitu vinabadilika tofauti na zamani, Dunia imekuwa Kijiji, vitu ambavyo vilikuwa vinafanyika nje sasa hivi vinaonekana.
Wataalamu, kozi zimeongezeka, zimefanyika kozi nyingi sana, za makocha, semina zinafanyika kwa Upande wa uongozi, vyote hivyo vikiwa na lengo la kuongezeana uwezo.
Tuliona juzi bodi ya ligi walikuwa na Waandishi, kulikwa na wasemaji mameneja, kwa hiyo wanajaribu kuongezea uwezo hawa ambao watu kwenye hii tasnia.
Kwaiyo mrejesho wake ndo haya mabadiliko tunayoyaona, zamani watu walikuwa wanakosa uwezo, watu walikuwa Wanakosa kufahamu vitu, lakini sasa hivi watu wanafahamu.
kwanini
Kwa maana ya Pre-season, hiyo nafiriki ndo topic inayoanzia hapo, kwa hiyo makocha wameelimika tofauti na zamani watu walikuwa waongoza vikundi (maana kuongoza timu ni lazima ufuate misingi na taratibu)