Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli amelitangazia taifa usiku wa kuamkia leo kifo cha aliyekuwa raisi wa Tanzania mzee wetu Benjamin William Mkapa.
Hakika hii ni huzuni kwa kila Mtanzania na mzalendo lakini kwa sisi watu wa soka mzee Mkapa atadumu mioyoni mwetu kila tukiutazama urithi alitouachia wa UWANJA WA TAIFA WA KISASA.
Wazo la uwanja huu wenye uwezo wa kuingiza watu 60,000 lilikuja katika awamu yake na mwaka 2005 uwanja huu ulianza kutengenezwa na kufunguliwa 2007 ikiwa moja ya viwanja bora sana barani Afrika.
PUMZIKA KWA AMANI (RIP) BENJAMIN WILLIAM MKAPA, NA ASANTE KWA ULIYOTUFANYIA.