Kijamii

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Lifestyle

SIL

MenuKijamiiMaoni
Articles

Msiingize siasa chanjo dhidi ya Covid-19'

3b8c5433eb6b760af149c234e0189e01 Msiingize siasa chanjo dhidi ya Covid-19'

Fri, 24 Sep 2021 Chanzo: www.habarileo.co.tz

MKUU wa Mkoa wa Tanga, Adam Malima, amewataka wataalamu wa afya kuacha kuingiza siasa katika kupeleka elimu ya kuhamasisha chanjo ya ugonjwa wa Covid-19 kwa wananchi.

Kauli hiyo aliitoa wakati wa kikao cha tathimini ya utoaji wa chanjo ya Covid-19 kwa wananchi wa mkoa huo. Alisema kuwa lengo la serikali ni kudhibiti maambukizi mapya hivyo chanjo hiyo ni vema walengwa wakaipata.

"Wataalamu wa afya kama mmeweza kuhamasisha wazazi kuna umuhimu wa kuchanja watoto wachanga, basi nendeni mkahamasishe watu umuhimu wa chanjo ili kuendelea kujikinga na ugonjwa wa Covid-19," alisema.

Aidha, aliwataka wanasiasa na viongozi wa dini kuendelea kutumia majukwaa yao kwa ajili ya kuelimisha wananchi kuona manufaa ya kuchanja ili kuendelea kujilinda na maambukizi mapya.

Akitoa takwimu za chanjo kwa mkoa huo, Mganga Mkuu wa Mkoa, Dk Jonathan Budenu, alisema lengo ni kuchanja walengwa 390,000 lakini wameweza kufikia watu 10,939.

Alisema kuwa bado wanaendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kutoa chanjo katika maeneo yenye mikusanyiko kama shuleni, sokoni, kwenye misikiti, makanisa pamoja na vyombo vya usafiri.

Aidha, aliongeza kuwa ili kusogeza huduma ya chanjo ya Covid-19 kwa wananchi wameanza kutoa huduma hiyo katika ngazi ya msingi kwenye vituo vinavyotoa huduma ya chanjo nyingine.

Columnist: www.habarileo.co.tz