Kijamii

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Lifestyle

SIL

MenuKijamiiMaoni
Articles

MZEE WA UPUPU: Manungu wameenda sasa ni zamu ya saa nane mchana

Simba Yanga Pic Manungu wameenda sasa ni zamu ya saa nane mchana

Wed, 9 Feb 2022 Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz

Mwaka 1976, Bob Marley aliachia albamu yake ya Rasta Man Vibration iliyokuwa na nyimbo kadhaa ukiwemo WAR (Vita) ambao uliakisi hotuba ya Mfalme Haile Selassie I wa Ethiopia kwenye Umoja wa Mataifa mwaka 1963.

Katika wimbo huo, Bob Marley aliimba kwamba dunia itaendelea kuwa na vita hadi pale usawa utakapokuwepo.

Until the philosophy that holds one race superior and another inferior (Ni hadi pale falsafa inayokumbatia tabaka moja kuwa juu na jingine kuwa chini). Is finally and permanently discredited and abandoned (Itakapofikia mwisho na kuachwa jumla).

That until there is no longer first class and second class citizens of any nation (Ni kwamba ni hadi pale patakapokuwa hakuna raia wa daraja la kwanza na daraja la pili wa nchi yoyote).

Hapa Bob Marley alitangaza vita duniani hadi mambo hayo na mengine mengi kama hayo yatapopatiwa ufumbuzi.

Kiasili maneno hayo yalisemwa na Haile Selassie I kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa, Oktoba 4, 1963, akihutubia kama mwenyekiti wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU). Hamishia maneno haya kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

Kwa miaka na miaka ligi yetu imekuwa na falsafa inayokumbatia tabaka moja juu na jingine chini. Tabaka la juu ni Simba na Yanga na tabaka la chini ni wengineo. Yaani ligi yetu imekuwa haina tofauti ni nchi yenye raia wa daraja la kwanza na daraja la pili. Simba na Yanga ni raia wa daraja kwa kwanza wengine ni daraja la pili.

KIVIPI?

Mambo mengi yanafanyika au yanatokea kwa faida ya Simba na Yanga yakiwakandamiza wengine. Kwa miaka na mikaka, Simba na Yanga hazikuwa zikilazimika kwenda kucheza kwenye baadhi ya viwanja eti kwa sababu zina mashabiki wengi.

Eti mashabiki wengi wanaweza kufanya fujo na kuwadhibiti itakuwa vigumu. Hivi ni shabiki gani angeweza kwenda kufanya fujo Mlandizi kwenye uwanja wa Ruvu Shooting ndani ya kambi ya jeshi?

Baada ya kilio cha muda mrefu cha hao raia wa daraja la kwanza, hao watu wanaokumbatiwa na falsafa na kuwaweka juu hatimaye wameenda kucheza huko. Wameanzia Manungu, wataenda Mlandizi, wangeenda Mwadui kama timu yao ingekuwepo...na kila sehemu kama hizo.

Kilichobaki sasa ni mechi za saa nane. Kama huo muda haufai, basi usifae kwa wote. Na kama unafaa basi na ufae kwa wote. Siyo wengine wakumbatiwe na falsafa kama raia wa daraja la kwanza na wengine daraja la pili.

Nilishawahi kuandika hapa, madhara ya mechi za saa nane mchana katika vita endelevu ni kubwa kuliko mchezo husika. Kucheza saa nane mchana kutamlazimu mchezaji kutumia nguvu nyingi zaidi ya kawaida kutoka akiba yake ya nguvu mwilini.

Matokeo yake atachoka sana siku zijazo, siyo katika mchezo husika pekee. Katika mbio za ubingwa zile timu ambazo hazikutani na hiyo adha wachezaji wake wanabaki na akiba ya nguvu na kuitumia mwishoni. Hii ni sayansi kwa hiyo kama imewezekana kwa raia hawa wa daraja kwanza kwenda Manungu na iwezekane pia kucheza saa nane au mechi za saa nane ziondolewe.

Columnist: www.mwanaspoti.co.tz