Kijamii

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Lifestyle

SIL

MenuKijamiiMaoni
Articles

Hisia mseto baada ya Kalonzo Musyoka kukutana na Muthama

E497174ecf9a5239 Hisia mseto baada ya Kalonzo Musyoka kukutana na Muthama

Mon, 26 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mwenyekiti wa UDA alikutana na kiongozi wa Wiper na mtandao ukasambaa hisia msetoChama cha UDA kinahusishwa na DP Ruto laikini mwenyekiti wake ni Muthama kutoka UkambaniTyari Muthama ametangaza kuwania ugavana Machakos eneo ambapo Wiper ndio huvuma chini ya kiongozi wake KalonzoHisia mseto ziliibuka mitandaoni Jumamosi Julai 24 baada ya mahasimu wa kisiasa kutoka Ukambani Johnson Muthama na Kalonzo Musyoka kukutana wakati wa hafla ya mazishi.

Wawili hao hao walionekana kwenye picha iliyopakiwa mtandaoni na maswali kuibuka iwapo wanapanga kuzika tofauti zao.

Picha hiyo ilizua mdahalo sana kwa sababu Muthama kwa sasa ni mwandani wa Naibu Rais William Ruto ambapo anahudumu kama mwenyekiti wa chama cha United Democratic Alliance (UDA).

UDA kinahusishwa na na DP Ruto huku akiwa ameweka wazi atakitumia kutafuta kura za kuingia Ikulu 2022.



Kabla ya kuingia kambi ya Ruto, Muthama alikuwa mwandani wa Kalonzo na aliaminika kuwa mfadhili wake wa kisiasa.



Read also

Wiper Yamfukuza Gavana Kivutha Kibwana wa Makueni Baada ya Kutawazwa Kuwania Urais

Kwa sababu ana mifuko mizito, Muthama alikuwa kiungo muhimu kwenye muungano wa NASA uliohusisha Kalonzo, Raila Odinga, Moses Wetangula na Musalia Mudavadi 2017.

Kufufuka kwa urafiki kati ya wawili hao inaweza kuwa pigo kisiasa kwa DP Ruto na chama chake cha UDA.

Tayari Muthama amefichua kuwa atawania ugavana wa kaunti ya Machakos ambapo aliwahi kuhudumu kama seneta.

Kalonzo na chama chake cha Wiper ndio wanawika katika siasa za Ukambani na maswali yanaibuka iwapo Muthama atatii na kuigia Wiper au ana nguvu ya kushinda kupitia tiketi ya UDA.

Siasa za Kenya huhusishwa na vigogo na kila eneo kuna vyama ambavyo huwa na wimbi linalowasomba wanaoenda kinyume.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Columnist: kiswahili.tuko.co.ke