Kijamii

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Lifestyle

SIL

MenuKijamiiMaoni
Articles

Gael Bigirimana, amka usingizini Wananchi watakuchoka

Gael Bigirimana 10 Kiungo wa Yanga, Gael Bigirimana

Wed, 19 Oct 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Pale mjini Shinagawa Nchini Japan wanajivunia mzee mmoja aitwaye Kurosawa Akira mtayarishaji wa Filamu mwenye tungo makini za Maisha, Yeye aliwahi kusema ‘Man is a genius when he is dreaming.” Mtu hutimamuka akiwa usingizini.

Yes, keti chini ewe Gael Bigirimana mume wa Mrembo Natalia Leigh, Nisikilize kwa makini kidogo. Najua Mpaka sasa umeshapata picha ya Ligi yetu, huku kwetu viatu vinagusa sana ngozi za miguu ya wapinzani. Hii ndiyo ligi inayohusudu nguvu na maarifa.

Hapo Yanga walipita viungo wenye sifa zote mbili, alikuwepo Thaban kamusoko aliyeiuita mpira na ukaitika, alikuwepo Pappy Tshishimbi aliyewasumbua wanalunyasi kila uchwao, Wote hawa walikuwa na ufalme wao hapo Jangwani, lakini wakaondoka. Lakini mpaka leo wanakumbukwa kwa mema yao.

Usingizi haujawahi kuisha ewe Gael Bigirimana mwana wa Mzee Bigirimana wa pale Bujumbura, amka sasa kwenye kitanda chenye godoro zito la GSM, amka uwapeleke wananchi kwenye hekaya lako la Newcastle ya England, amka uwakumbushe mema yako.

Imani ya wananchi wengi ni kwamba unaweza wakumbusha zile pasi za Babu Chuji mbele ya Anko Ngasa wakati Ule, pengine ukawarudisha enzi za mbrazil Coutinho aliyeng’ara mpaka CCM Kirumba Mwanza, amka uutambarize mpira kama ulivyoutambariza pale Stade Prince Louis Rwagasore Kwenye baraka za wazee wako.

Gael Bigirimana Bado miguu yako haijazungumza na wananchi, Bado kichwa chako hakijawaliwaza wananchi, bado jasho lako halijawakosha wananchi, amka sasa Gael, amka kitandani Mwamba, amka ewe mfalme, usisubiri kitanda chako kitiwe Maji ili uamke, amka mwenyewe muafrika uliyeng’ara Ulaya. Ukisibiri embe iive, Aucho anazidi kula na Chumvi.

Imeandikwa na Abdulazeez Kipanduka.

Columnist: www.tanzaniaweb.live