Mrembo kutoka WCB, Zuhura Othman ameteuliwa kuwania tuzo kubwa duniani za MTV EMA ambapo ametajwa katika kipengele cha Best African Act (Msanii Bora wa Afrika-2022).
Kwenye tuzo hizo, Zuchu atachuana na mastaa wakubwa wa Afrika Burna Boy (Nigeria), Ayra Starr (Nigeria), Musa Keys (Afrika Kusini) na Black Sherif wa Ghana.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zuchu amewashukuru mashabiki wake kwa kuchangia mafanikio hayo makubwa.
“Tanzania stand up your girl is nominated on the MTVEMA, god is good niseme asante ni kwa sababu yenu ndo mimi niko hapo nawapenda sana im coming back with a better caption cos right now am still shaking let me calm down first,” aliandika Zuchu.