Mwanaharakati wa masuala ya mitandao Carry Mastory amesema kuwa kwa sasa msanii wa Bongo Fleva kutoka Lebo ya WCB, Zuchu hawezi kuolewa na Diamond.
Carry amesema hayo wakati akihojiwa na chombo kimoja cha habari alipoulizwa kuhusu mahusiano ya Diamond na Zuchu.
"Zuchu hawezi kuolewa, angekuwa anaweza kuolewa basi Diamond angeshamuoa kitambo. Kuna post moja Romy Jones alimtania Zuchu, lakini nikaona Mama ameandika kabisa kwa hisia;
"...‘Kwa miaka mine nilikuwa namuomba Diamond amsaidie mwanangu, ndiyo anamsaidia huku anamchezea tena?’ inamaana mama mwenyewe hafurahishwi na kinachoendelea mitandaoni," amesema Carry.