Zuchu; ni malkia mwingine wa muziki wa Kizazi Kipya nchini Tanzania, ambaye analia na kusikitishwa na kitendo cha paka wake kupachikwa mimba ilihali yeye hana.
Zuchu ambaye kumekuwa na tetesi kuwa anatoka kimapenzi na bosi wake Diamond Platnumz anasema kuwa, kitendo hicho kimemdhalilisha kwa kuwa ataonekana hajui kulea.
“Yaani paka wangu wameshampa mimba sasa hivi, mimi mama yake sina mimba, lakini yeye amepata mimba, kwa nini? Amenidhalilisha sana, ninaonekana mama gani mimi ambaye sijui kulea,” anasema Zuchu.
Baadhi ya wafuasi wake, naye wamemuomba ambebee mimba Diamond maana akichelewa sana atakuta mwana si wake.