Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Zuchu amtisha Yemi Alade

Zuchu 34zuchu New.png Zuchu na Yemi Alade

Sat, 9 Apr 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

ZUHURA au Zuchu ni malkia mpya wa Bongo Fleva anayeitumikia Lebo ya WCB ambaye ameweka rekodi nyingine baada ya kutinga kwenye nne bora ya wanamuziki wa kike kutoka barani Afrika wenye ufuasi mkubwa kwenye mtandao wa YouTube akimtisha Yemi Alade wa Nigeria.

Zuchu ambaye ametajwa kama mwanamuziki anayekua kwa kasi ya ajabu kimuziki tangu kutambulishwa kwenye lebo ya WCB mwaka 2020, amefikisha wafuasi milioni 1.9 kwenye YouTube hivyo kuwa mwanamuziki wa kike wa nne barani Afrika kupata idadi hiyo ya wafuasi.

Namba moja inashikiliwa na Sherine kutoka Misri ambaye amejizolea wafuasi zaidi ya milioni 4.22, anafuatiwa na Zina Doudia kutoka Morocco akiwa na wafuasi milioni 3.04 kisha Malkia wa Afrobeats kutoka Nigeria, Yemi Alade akiwa namba tatu na wafuasi milioni 1.96

Sasa Zuchu kutoka Tanzania ana wafuasi zaidi ya milioni 1.9 akitazamia kumpiku Yemi Alade muda wowote.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live