Huu ni mpambano usio rasmi. Kwa nyakati tofauti, muigizaji Irene Uwoya na Sosholaiti Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ wametupia picha ambazo zimeonesha sehemu kubwa ya miili yao ikiwa tupu.
Uwoya ndiye aliyekuwa wa kwanza kutupia picha hiyo jana katika akaunti yake ya Instagram ambapo alikuwa amevalia kizibao flani huku blaa yake pamoja na nguo ya ndani ikionekana live bila chenga huku akionekana kwa mbale.
Saa chache baadaye, Zari naye aliibuka kwenye ukurasa wake wa Instagram na kutupia picha inayomuonesha akiwa amevalia kigauni flani hivi kilichomuacha mgongo wake mzima wazi na kama hiyo haitoshi, kacheni kake ka kiunoni kaliweza kuonekana pia.
Wadau mbalimbali wamekuwa na mtazamo tofauti juu yao. Zari ana umri wa miaka 41 huku Uwoya akiwa na 33. Usisahau, hao wote wamewahi kutembea na Diamond. Zari alizaa naye watoto wawili, Uwoya ilikuwa ni kupita njia tu.
Wewe mdau wa www.tanzaniaweb.com una lipi la kusema? Tupia komenti zako hapo chini.