Msanii ZaiiD amesema kutokana na ngoma yake ‘Wowowo’ kufanya vizuri amefanya show takribani mikoa yote Tanzania.
ZaiiD amesema kutokana na kufanya show hizo ndipo kumepelekea kukaa kipindi kirefu bila kutoa ngoma nyingine tangu alipotoa Wowowo.
“Mpaka ninavyongea hapa almost nimeshazunguka mikoa yote, kama basi umebaki mmoja au miwili lakini nimezunguka Tanzania nzima lakini kila mkoa nikienda nafanya show zaidi ya nne au tano,” ZaiiD ameiambia Clouds Fm.
ZaiiD amesema kwa sasa hadi tayari ameshaona fanya video tatu bado kuzitoa tu. Utakumbuka ngoma ‘Wowowo’ alitoka August, 2017, video yake sasa ina views zaidi ya milioni 1.2 katika mtandao wa YouTube.