Rapa Young Lunya amefunguka kuhusu madai ya stori zinazosemekana kwamba anatoka kimahusiano na staa wa filamu Irene Uwoya kwa kusema kama taarifa hizo zingekuwa na ukweli ingeshajulikana.
Submitted by Shaluwa Anta on Jumapili , 13th Jun , 2021 Picha ya msanii Young Lunya na Irene Uwoya
Akizungumzia madai ya stori hizo zinazoendelea kwenye mitandao ya kijamii Young Lunya amesema "Ingekuwa ni kweli basi ingeshajulikana, uzuri ni kwamba mahusiano sio kitu cha kufichika".
Hii sio mara ya kwanza kwa Young Lunya kusemekana kwamba ana mahusiano na mastaa wa kike kwani kipindi cha nyuma zilitoka stori zinazosema ana-date na Mimi Mars pamoja na Barbiemia.
Zaidi mtazame hapa chini akizungumzia hilo.