Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Young Killer amvuruga Diamond

KILLER MONDI Young Killer amvuruga Diamond

Wed, 12 Jul 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Rapper @youngkillermsodokii ni kama amevuruga mipango ya msanii @diamondplatnumz aliyokuwa amejiwekea ya kukaa namba moja kwenye Trending YouTube kuanzia Julai hadi ifikapo Januari 2024.

Kupitia Freestyle Session 6 ya Msodoki iliyoachiwa Julai 10, ambayo amemchana rapper @younglunya imeishusha 'Baby' REMIX hadi namba mbili na yeye kukaa namba moja kwenye nyimbo zinazofanya vizuri zaidi Tanzania (Popular Right Now).

Wakati huo huo, Msodoki kwenye Trending (For Music) anashika namba 4 na 'My Baby' bado ipo namba moja huko YouTube huku Freestyle Session 5 ya Lunya ikiwa namba tatu.

Huwenda @diamondplatnumz akarejea tena namba moja kwenye nyimbo zinazofanya vizuri zaidi Tanzania (Popular Right Now) YouTube kupitia mikwaju yake hiyo ambayo bado inafanya vizuri.

Mapema leo asubuhi @diamondplatnumz ameachia video ya wimbo wake 'Shu' aliomshirikisha @chley_nkosi lakini pia nikukumbishe kuwa wawili hawa miaka minne iliyopita walishirikiana kwenye ngoma iitwayo 'Pamela'.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live