Menu ›
Burudani
Fri, 12 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkali wa michano, Young D amesema kwa sasa yupo singo kwa maana hana mchumba au mpenzi wa kueleweka.
Young amefunguka hayo kupitia radio Wasafi alipofanya mahojiano hivi karibuni ambapo aliulizwa nyumbani kwake anaishi na nani ndipo aliposema, anaishi na mwanaye na dada wa kazi pekee.
“Mimi nipo singo, naishi na mwanangu pamoja na dada wa kazi tu. Ila sio kwamba sina kabisa mtu lakini kifupi nipo singo,” alisema Young D.
Hata hivyo, Young D aliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na sosholaiti Tunda lakini hata hivyo waliachana na mrembo huyo akaweka kambi kwa Whozu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live