Dar es salaam. Mwanamuziki na mnenguaji nguli mwenye asili ya Kongo Yondo Sister kutumbuiza nchini Kenya na Tanzania.
Akizungumza na gazeti la Daily Nation jijini Nairobi Kenya, amesema licha ya kuwa hakupanga kufanya shoo katika nchi hizo kwa sababu yupo likizo nchini Kenya, itamlazimu kufanya shoo Kenya na Tanzania ili kuungana na mashabiki zake wapya na wa zamani.
Takribani miaka 24 tangu mwanamuziki huyo alipotembelea nchini humo alisema baada ya kuwasili jijini Nairobi siku ya Jumatano anatamani kuonana na mashabiki zake wa zamani.
Mashabiki wa mwanamama huyo anayetamba na miondoko ya bolingo wa nchini Kenya watapata nafasi ya kumuona katika uzinduzi wa Tembo hoteli siku ya Ijumaa atakapo kuwa mgeni rasmi katika tamasha hilo la uzinduzi.
“Ingawa sikupanga kufanya onyesho lolote nikiwa likizo bado naangalia uwezekano wa kufanya shoo katika nchi hizi mbili, ”amesema.
Katika uzinduzi wa hoteli hiyo, Yondo Sister atasindikizwa na wasanii wa bendi za muziki wa Kikongo nchini Kenya ikiwamo Mangelepa inayoongozwa na mwimbaji na mtunzi mkongwe Kabila Kabanze “Evan.”
Pia Soma
- Gabo: Tupendane tukiwa hai
- Mlela: Ninapenda maisha ya kiki
- Yusuph Mlela asema hana uhusiano wa kimapenzi na Ebitoke