Mwimbaji na mtunzi maarufu wa nyimbo kutoka Nigeria Yemi Alade anasema amenusurika kwenye ajali ya gari alipokuwa nchini Uhispania.
Katika chapisho kwenye Instagram yake Jumanne,msanii huyo alifichua kuwa ajali hiyo ilitokea Alhamisi iliyopita akiwa safarini kati ya Barcelona na Benicassim.Hakuna vifo vilivyoripotiwa.
Alisema ajali hiyo "ilitokea ghafla" lakini alipata majeraha madogo,.
Alade, anayejulikana kwa muziki wake wa kusisimua, alisema licha ya ajali hiyo bado alitumbuiza jukwaani saa chache baadaye siku hiyo hiyo, kisha akapata "dharura ndogo ya matibabu" .
Alimshukuru Mungu kufuatia shida yake, akisema "Neema yake inatosha".