Menu ›
Burudani
Sun, 28 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Supstaa wa Bongo Movies, Jackline Worlper na mpenzi wake ambaye ni mfanyabiashara Rich Mitindo wameendelea kukuza familia yao.
Hii ni baada ya wawili hao kufanikiwa kupata mtoto wa pili ambapo Wolper amejifungua hivi karibuni mtoto wa kike.
Itakumbukwa, mapema mwanzoni mwa mwezi huu wa Agosti, Wolper na Mitindo walitangaza rasmi kwamba walikuwa wanatarajia mtoto wa pili katika familia yao.
Wawili hao tayari wameshatangaza tarehe ya ndoa yao ambayo itakuwa Novemba mwaka huu 2022.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live