Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wimbo Uno wa Harmonize waondolewa Youtube, walioutayarisha wazungumza

85216 Pic+uno Wimbo Uno wa Harmonize waondolewa Youtube, walioutayarisha wazungumza

Fri, 22 Nov 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Wimbo Uno wa msanii wa Tanzania, Rajab Abdul maarufu Harmonize umeibua utata na kuondolewa katika mtandao wa Youtube.

Umeondolewa na Magix Enga, mtayarishaji wa muziki nchini Kenya anayedai kuwa mdundo wa wimbo huo uliotoka takribani mwezi mmoja uliopita, ni wake.

Novemba 17, 2019  Enga alimuomba Harmonize kuufuta wimbo huo katika mtandao huo na kumpa wiki moja na kuahidi kuwa asipofanya hivyo, atachukua jukumu hilo mwenyewe.

Enga amesema mdundo wa wimbo huo umefanana na wimbo wa Dundaing alioutengeza.

Mwananchi lilimtafuta Harmonize na meneja wake kuzungumzia suala hilo bila mafanikio kutokana na simu zao kutokuwa hewani huku watayarishaji wa wimbo wa Uno, Hunter na Bonga wakitoa maoni tofauti kuhusu suala hilo.

“Mimi nilifanya ‘mixing’ za huo wimbo, kuandaa mdundo alifanya Hunter G, muulize yeye ndio ana majibu mazuri ya suala hilo,” amesema  Bonga.

Kwa upande wake Hunter amesema, “sijawahi kuiba mdundo wa wimbo wowote katika maisha yangu. Midundo huwa inafanana kwa kuwa unaweza kutumia kinanda au kifaa chochote.”

“Ninachojua mdundo wa wimbo wa Uno nimeutengeneza mwenyewe sijachukua kwa mtu yeyote. Nimefanya kazi nyingi za kuwatengenezea wasanii midundo ya nyimbo zao kama Juliana Kanyomozi, Bushoke na Christian Bella.”

Endelea kufuatilia Mwananchi kwa taarifa zaidi

Chanzo: mwananchi.co.tz