Mpenzi wa sasa wa mwanamuziki Oscar John Lelo ‘Whozu’, Wema Isack Sepetu ndiye staa wa kike Bongo ambaye ameweka rekodi ya kusukuma ndinga za kifahari kwa miaka 10 mfulululizo tangu alipotwaa taji la Miss Tanzania mwaka 2006 hadi 2016 na mpaka sasa hakuna aliyevunja rekodi hiyo.
Kwa sasa Wema haifahamiki anatumia gari aina gani licha ya mara mwisho kuposti picha mtandaoni akiwa amepozi mbele ya Toyota Harrier Hybrid, moja kati ya magari ya kifahari.
Baadhi ya magari ambayo aliyaendesha mdada huyu ambaye ‘hazeeki’ na bado analipa licha ya kujikondesha ni TOYOTA LEXUS (Mil. 32), TOYOTA MARK X ( Mil. 38), AUDI Q7 (Mil.80), BMW 545i ( Mil.56), NISSAN MURANO (Mil. 36) na RANGE ROVER EVOGUE (Mil. 140).
Je, ni staa gani wa kike kwa sasa ambaye unaona ana mzuka wa kupenda magari ya kifahari?