Filamu inayosubiriwa kwa hamu kubwa na watu wengi Ulimwenguni "Wednesday" imetangazwa kuanza uzalishaji wake kwa Season 2 huko nchini Ireland.
Netflix Leo jumanne imetangaza majina kadhaa mapya ya waigizaji watakao jiunga na wengine katika mfululizo huu, Waigizaji maarufu kama Steve Buscemi (The Big Lebowski, Boardwalk Empire), Billie Piper (Scoop, I Hate Suzie) na wengine wengi wamo ndani.
Wednesday ni FIlamu ya kutisha (Horror series) inayofanya vizuri tangu kuachiliwa kwake mwezi Novemba 2022, ikiwa na mauzo makubwa kote Ulimwenguni ikishindanishwa na FIlamu kama "Stranger things".
Je, Uliikubali kwa asilimia ngapi hii FIlamu?