Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watu 100 wajiua baada ya kusikiliza wimbo huu

Gloomy Sunday (18).jpeg Watu 100 wajiua baada ya kusikiliza wimbo huu

Tue, 7 Nov 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Gloomy Sunday (Jumapili ya Huzuni) ni wimbo uliotungwa na Rezso Seress (Rudi Spitzer), msanii kutoka nchini Hungary mwaka 1933. Reszo alitunga maneno ya wimbo huo na kupiga mwenyewe ala ya huzuni ya wimbo huo, baada ya kuachwa na mpenzi wake

Inaelezwa kwamba kitendo cha kuachwa na mwanamke aliyekuwa akimpenda sana, kilimfanya apatwe na huzuni kali na msongo wa mawazo, na katika kipindi hicho ndipo alipopata wazo la kutunga mashairi na baadaye kuutengeneza wimbo huo.

Kwa sababu aliuimba akiwa na huzuni kali, wimbo nao ulijawa na hisia kali, za mtu anayelalamika kuvunjwa moyo na mpenzi wake, akifananisha kitendo cha kuachwa kuwa sawa na kufiwa na mpenzi aliyekuwa anampenda.idk_1.png

Awali ulionekana kuwa wimbo wa kawaida wa huzuni, lakini matukio ya watu kuyakatisha maisha yao baada ya kuusikiliza mara nyingi wimbo huo kwa kuurudiarudia yalianza kuripotiwa, wengine wakiacha kabisa ujumbe kwamba wamejiua baada ya kusikiliza wimbo huo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live