Menu ›
Burudani
Mon, 19 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Muigizaji wa sinema za Kibongo, Wastara Juma, amesimulia kuwa kuna wakati aliwahi kunywa sumu ili kujiua.
Wastara alisema kwenye maisha yake amepitia nyakati hizo mara mbili kutokana na maneno ya watu.
“Kuna wakati nilitaka kufanya hivyo wakati naumwa halafu watu wanazusha maneno ya uongo, lakini pia huko nyuma niliwahi kunywa vidonge vya dawa vingi ili nife.
“Nilikuwa na miaka 14 nikiwa mjamzito na mtu ambaye simpendi, niliozeshwa kilazima,” alisema Wastara.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live