Menu ›
Burudani
Sat, 8 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Muigizaji wa filamu na tamthiliya za Kibongo, Godliver Gordian amesema kati ya vitu ambavyo vinawatafuna wasanii wengi wa Bongo ni nidhamu.
Amesema wasanii wengi hususan wale maarufu, wamekuwa wakipunguza nidhamu ya kazi tofauti na wasanii wakubwa wa nje.
“Tunahitaji kuwa na nidhamu ya kazi. Wasanii na wazalishaji wa kazi. Vitu vinavyotushinda wasanii wengi ni nidhamu na tuwe na imani. Mimi nishafanya kazi na wasanii wa kimataifa, unaoona wanakuwa na nidhamu sana tofauti na sisi,” alisema Godliver bila kuwataja majina
Chanzo: www.tanzaniaweb.live