Menu ›
Burudani
Wed, 15 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wasanii wanaotumia dawa za kulevya watakiwa kujirekebisha, kabla hatua juu yao hazijachukuliwa.
Hayo yamesemwa jana Novemba 14, na Aretas Lymo ambaye ni Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kupambana na Kudhibiti dawa za Kulevya, wakati akizungumza na wanahabari na wahariri.
Aretas Lymo amesema wapo wasanii wanaotumia Cocaine, Heroine na Bangi, na wapo wanaohamasisha matumizi ya dawa hizo hivyo wakithibitishwa sheria itafata mkondo wake.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live