Wakazi wengine wa Kigamboni amemwomba Rais Magufuli na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda wasaidiwe kurudishiwa uwanja wao ambao wamedai kudhurumiwa na Bwana Michael Kagembe na Mohammed Mtundwi, tangu mwaka 1995 ambayo inadaiwa kuwa ni familia ya akina Z Anto.
Akizungumza na Waandishi wa Habari mapema Jumapili hii, jijini Dar es salaam Bi.Rukia Mbaraka Saidi amesema alianza kufuatilia kesi aliyoifungua tangu mwaka 1995 mpaka leo bila kupata haki yake licha ya kesi kushinda.
Baada ya taarifa hiyo, Bongo5 iliitafuta familia ya Z Anto na kusema siku ya leo itatoa ufafanuzi juu ya malalamiko hayo yote.