Rapper kutoka kundi la SSK, Wakazi ameweka wazi tarehe ya kuachia albamu yake ya ‘KISIMANI’ yenye ngoma 18.
Wakazi anayetamba na ngoma yake ya ‘Bakora’ ametaja tarehe 16, mwezi Machi mwaka huu kuwa ndoyo siku atakayotoa albamu yake hiyo ya ‘KISIMANI’ aliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu.
Albamu ya ‘KISIMANI’ imetayarishwa na maproducer 12 tofauti na kuwashirikisha wasanii wa muziki wa Bongo flava wa RnB, Hip Hop na raggge.
Tarehe 16 mwezi Machi, Tanzania itakuwa ikishuhudia ujio wa albamu mbili za wasanii wake ambao ni Diamond Platnumz n albamu yake ya ‘A Boy From Tandale’ na ‘KISIMANI’ ya rapper Wakazi