Vera Sidika ameweka wazi mahusiano yake na njemba ambaye amekuwa akimpost mara kwa mara kwenye mitandao yake ya kijamii.
Mrembo huyo kutoka Kenya, amekuwa akiibua maswli mengi kwa mashabiki kuhusu picha anazopiga na jamaa huyo.
Lakini jumatano hii ikiwa ni sikukuu ya Valentine’s Day, Vera ameonyesha kuwa na mahusiano ya kimapenzi na jamaa huyo mwenye asili ya kizungu baada ya kuachana na ex wake raia wa Nigeria.
“Happy Valentine’s Day from my BFF & I,” ameandika Vera kwenye picha hiyo hapo juu aliyoiweka kwenye mtandao huo.
Hizi ni picha nyingine ambazo Vera amewahi kupost akiwa na mzungu huyo.