Msanii wa Nigeria Tems ameshutumiwa kwenye mitandao ya kijamii kwa vazi lake ambalo lilizuia kuonekana kwa wahudhuriaji wengine kwenye Tuzo za Oscar.
Tems, 27, ambaye jina lake halisi ni Temilade Openiyi, aliteuliwa kwa Wimbo Bora wa Kiasilia wa wimbo wa Black Panther: Wakanda Forever Lift Me Up.
Gauni lake jeupe lililokuwa limezunguka kichwa chake lilishutumiwa baada ya picha ya skrini kuonyesha mgeni akikunja shingo yake ili kutazama jukwaa.
Wengi kwenye mitandao ya kijamii walimkosoa mwimbaji huyo kwa kuwa "mkorofi".
Nguo ya Tem ilishonwa na mwanamitindo mzaliwa wa Ukraine- Lessja Verlingieri wa Lever Couture.
Msanii huyo alishinda Tuzo za Grammy mwezi Februari katika kitengo cha Best Melodic Rap Performance kwa mchango wake kwenye wimbo wa Wait for U akiwa na Future na Drake.