Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Vanessa Mdee kuachia albamu mpya chini ya Universal Music Group

389 24174941 175298819725151 2611836777396174848 N TZW

Tue, 19 Dec 2017 Chanzo: bongo5.com

Baada ya dhiki ni faraja. Vanessa Mdee afunguka kuachia albamu yake mpya mwakani chini ya Universal Music Group.

Vee Money amesema hilo baada ya kutangaza kusaini mkataba na kampuni hiyo kubwa ya muziki duniani ambayo itakuwa inasimamia kazi zake katika Ulaya na Afrika.

Akiongea na Social Buzz ya Clouds TV, muimbaji huyo amesema albamu hiyo itatoka mwezi wa sita mwakani chini ya kampuni ya Universal ambapo kwa mkataba wa aina yake ambao amesaini unamfanya kuwa msanii wa kwanza kutoka Afrika kupata dili nono kama hilo katika kampuni hiyo.

Msanii mwengine wa Bongo Flava ambaye anafanya kazi na kampuni ya Universal ni Diamond Platnumz.

Chanzo: bongo5.com