Mtindo wa wasanii wa kubadili rangi za nywele umezidi kushika kasi, alianza Ben Pol kisha Alikiba na Ommy Dimpoz na hatimaye leo tumeona hilo kwa Vanessa Mdee.
Ben Pol ameonyesha kuvutiwa zaidi kwa hatua hiyo ya Vanessa kwani mwanzoni alipobadili zake wengi walimkosoa ila sasa mtindo huo umeanza ku-trend. Kupitia Instagram yake Ben Pol ameandika;Happy Faraja Week, naendelea kufarijika tu Vanessa Mdee.
Utakumbuka siku moja iliyopita Ben Pol alifanya kitu kama hicho mara baada ya kuona Alikiba na Ommy Dimpoz wamefanya hivyo. Wasanii wote kwa ujumla wameungana na wasanii wengine kama Harmonize, Queen Darleen, Lava Lava na Amber Lulu ambao walifanya hivyo awali.