Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

‘Valentines Day Surprise” Binti wa chuo ampa Mpenzi wake zawadi ya Mercedes Benz

Thu, 22 Feb 2018 Chanzo: millardayo.com

What is Love !! Kila mtu anaweza kutafsiri kwa njia tofauti tofauti ila wengi wanakubali kuwa ni hisia kali zenye Upendo Leo February 14, 2018 ni ‘Valentines Day’ sasa Binti mmoja amempa amempa ‘surprise’ mpenzi wake wa kiume kwa kumnunulia gari mpya aina ya Mercedes Benz katika siku ya leo ya wapendanao ‘valentines day’ nchini Kenya

Binti huyo aliyejulikana kwa jina la Fridah Kariuki ambaye ni mwana mitindo aliamua kumnunulia Michael Musyimi ambaye ni mpenzi wake zawadi hiyo kama ishara ya upendo wake kwake.

Fridah Kariuki mwenye umri wa miaka 20 ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Methodist nchini Kenya (KeMU) ambaye amesema, alimkopa baba yake fedha kwaajili ya kumnunulia mwanaume wake huyo gari alililokuwa akilitamani siku zote.

Wawili hao wanaopendana wamekuwa katika uhusiano huo kwa miaka minne na wamesema wanampango wa kuishi pamoja. Licha ya mshangao huo wawili hao wameweka wazi kuwa uhusiano wao huo unapewa ushirikiano wa karibu na wazazi wao.





Chanzo: millardayo.com