Dar es Salaam. Mwili wa msanii wa muziki nchini Tanzania, Abdallah Matimbwa maarufu ‘Mbalamwezi’ utazikwa kesho Jumamosi Agosti 17,2019 kabla ya saa 6 mchana.
Ally Mponda ambaye ni mjomba marehemu akizungumza na Mwananchi leo Ijumaa Agosti 16,2019 amesema hatua ya kuamua kuuzika mwili huo mapema unatokana na kuharibika.
Mponda amesema maziko hayo yanatarajiwa kufanyika kati ya makaburi ya Kamla au Kilimahewa yaliyopo Tandika Jijini Dar es Salaam.
"Tumemuona Dula ameharibika sana, hivyo tusingependa kuuweka mwili wake muda mrefu, inawezekana tukamzika saa nne na tumechelewa sana haitazidi saa sita," amesema Mponda.
Akielezea kuhusu taarifa za kupotea kwake, amesema marafiki zake wamesema hawakumuona tangu sikukuu ya Iddi na hii ni baada ya kumuacha kwenye nyumba wanayoishi na wao kwenda zao kwenye shoo.
Siku hiyo, amesema Mbalamwezi alikataa kwenda na wenzake na kubaki nyumbani lakini baadaye waliporudi hawakumkuta.
Habari zinazohusiana na hii
- VIDEO: Kifo cha Mbalamwezi wa kundi la The Mafik chazua utata, ndugu wataka uchunguzi
- Msanii wa muziki Tanzania afariki dunia