Dar es Salaam. Msanii maarufu wa Tanzania, Diamond Platnumz amewazawadia magari ya kifahari mama yake mzazi, Sandra pamoja na mpenzi wake, Tanasha Donna katika siku yao ya kuzaliwa jana Jumapili Julai 7, 2019.
Diamond aliwakabidhi wawili hao katika iliyomalizika usiku wa kumakia leo Jumatatu sherehe aliowaandalia wawili hao iliyofanyika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam nchini Tanzania na kuhudhuriwa na watu mbalimbali.
Gari hizo aina ya Landcruser Prado, zinaelezwa kila moja kuwa na thamani isiyopungia zaidi ya Sh160 milioni.
Diamond aliwakabidhi wawili hao gari hizo saa 8:00 usiku wa kuamkia leo baada ya kuisha kwa sherehe hizo ambapo magari hayo yaliegeshwa nje.
Magari hayo yalibandikwa namba yakisomeka majina ya 'mama Dangote' ambaye ni mama yake mzazi na lile la mpenzi wake likiandikwa 'Tanasha.'
Wa kwanza kukabidhiwa gari alikuwa mama yake mzazi aliyemfungilia mlango kisha akahamia kwa Tanasha.
Pia Soma
- Mtangazaji anayedaiwa kuhusika katika mauaji Kenya aacha kazi
- Dk Kigwangalla ampoza Makamba mtandaoni
- TRA: Hatujapata tatizo stempu za kielektroniki
Mbali ya kupata zawadi hiyo ya gari, awali wakiwa ukumbini wawili hao walipewa makasha saba ambayo kulikuwa na zaidi mbalimbali kila mmoja alitakiwa kuchagua moja.
Katika kuchagua huko, Tanasha alishinda nyumba huku mama yake mzazi, Sh10 milioni ambazo hata hivyo ilielezwa watagawana milioni tano tano na Tanasha.