Menu ›
Burudani
Sat, 18 Jun 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Muigizaji Irene Uwoya, ametamba kuwa kutokana na umaarufu wa rafiki yake Kajala Masanja, siku akiolewa atamgharamia mavazi mwanzo hadi mwisho wa shughuli.
Uwoya amefunguka hayo mara baada ya kukabidhiwa ubalozi wa duka la mavazi ya maharusi lilipo Sinza jijini Dar.
"Kajala yule ni staa mkubwa sana, nitamgharamia kila kitu siku ya harusi yake kuanzia mwanzo mpaka mwisho nitasimamia shoo," alisema Uwoya.
Kajala amerejesha penzi mototo kwa Harmonize ambaye waliachana kwa muda mrefu na sasa wawili hao huwenda wakaanza kuifikiria ndoa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live