Menu ›
Burudani
Tue, 4 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nyota wa R&B Usher Raymond amepokea tuzo maalum ya heshima ya mafanikio ya kazi yake ya muziki (LIfetime Achievement) kupitia Tuzo za BET 2024.
Mbali na tuzo hizo mkali huyo yupo kwenye vipengele Vinne vya tuzo hizo (Album of the year), (Best Collaboration), (Best Male R&B/Pop Artist na Video of the Year)
Utoaji wa tuzo hizo unatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Peacock Threatre mjini Los Angeles nchini Marekani June 30, 2024.
Usher ataungana na wakali wengine waliopata heshima ya Tuzo hiyo kama vile Chaka Khan, Mary J, Blige, Busta Rhymes, LIonel Richie, P Diddy na wengine.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live