Menu ›
Burudani
Thu, 6 Jun 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwigizaji Mkongwe wa Bongo Movie Wastara Juma kupitia ukurasa wake wa Instagram amekanusha taarifa za kifo chake ambapo kuanzia siku ya jana baadhi ya kurasa mbalimbali zilikuwa zikichapisha habari kuwa Mwigizaji huyo amefariki.
Wastara amefunguka kuwa bado yupo hai hivyo watu wapuuze taarifa hizo.
Ikumbukwe hivi karibuni Mwigizaji huyo amekuwa akieleza kwamba kwa maumivu na shida anazopitia anatamani afariki.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live